BIBLIA INATOA MWANGA NA MWONGOZO WA KIROHO KATIKA MAENEO MBALI MBALI YA MAISHA YETU
Kiapo mahakamani hata Wabunge hutumia biblia katika kuapa.Ikiwa umeshauri wa nje ya neno la Mungu basi bila shaka utakuwa umepotoshwa.
biblia ni kitabu kinachofaa sana kwa ushauri.kitabu hiki kina mafundisho mengi sana yanayoonyesha,maisha,mafundisho na hekima ya Mungu.kitabu cha mithali kina mafundisho mengi ya hekima,busara,maadili na uongozi maishani.kitabu hiki pia kina maelekezo ya jinsi ya kuishi maisha ya furaha,amani na mafanikio.
Biblia pia ina kitabu cha zaburi ambacho ni mkusanyiko wa nyimbo za kusifu na kuabudu.Nyimbo hizi zinatoa faraja,nguvu na matumaini kwa watu wakati wa shida na mateso ;pia katika kitabu.cha zaburi tunaweza kupata mifano ya maombi na sala ambazo zinaweza kutusaidia katika ushauri na kumwomba Mungu.
Katika agano jipya tunapata mafundisho na mifano ya Yesu kristo..Ambaye ni mfano bora wa upendo,uhuru,msamaha na haki.mafundisho yake yanaweza kutufundisha katika kutoa ushauri nzuri na wa busara kwa wengine.pia kuna barua za mitume na mafundisho mazuri juu ja kujenda mahusiano mazuri.kuishi kwa haki na kumsifu Mungu katika maisha yetu
Biblia inatoa mwanga na mwongozo wa kiroho.katika maeneo mbalimbali ya maisha yetu,ikiwemo pamoja na masuala ya familia,ndoa,kazi,urafiki,fedha na maamuzi muhimu inatufundisha jinsi ya kuishi maisha ya maana yanayosikiliza na kumtii Mungu.Hivyo biblia ni chanzo kizuri cha USHAURI.
nimekuandikia haya ili imani yako isipukue katika bwana-Pastor James.
+225692076903.
Utakubaliana na na mimi kuwa biblia ni mwongozo hai wa maisha yetu.
ReplyDelete